Kauli ya Trump Yazua Utata, Yatajwa Kuvuruga Amani

Kauli ya Trump Yazua Utata, Yatajwa Kuvuruga Amani
Wakati mgogoro wa Marekani na Korea ya Kaskazini ukiwa bado unarindima, tishio jingine limeibuliwa na kauli tata aliyoitoa rais Trump siku chache zilizopita.

Katika kauli hiyo, Trump amenukuliwa akisema kuwa, anautambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa taifa la Israel.

Tayari wapalestina wamenza kuchoma moto picha za Trump kwa madai ya kukasirishwa na kauli yake hiyo.

Nayo Saudi Arabia imelaani hatua ya Marekani kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel. Katika taarifa yake, taifa hilo limesema kitendo hicho si cha haki.

Mgogoro wa Israel na Parestina umedumu kwa miongo kadhaa huku Marekani na Uingereza zikitajwa kuwa miongoni mwa vyanzo vya mgogoro huo.

Pande zote mbili, Palestina na Israel zimeendelea kuung’ang’ania mji wa Jerusalem kwa sababu mji huo una historia kubwa katika imani ya Kikristo na Kiislamu.

Wachambuzi wa siasa za Palestina na Israel wameonya kuwa, kauli ya Trump inaweza ikasababisha umwajikaji wa damu kuliko inavyotarajiwa.

Chanzo cha mgogoro wa Palestina na Israel, historia ya jamii hizo na imani tofauti za kidini zinafanya iwe vigumu kutoa suruhu.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne