BARCELONA YAKUMBWA NA SHAMBULIO LA UGAIDI
Askari wakiwa eneo la tukio |
Basi dogo limeripuka katika
kundi la wapita njia Barcelona, Hispania. Mlipuko huo umesababisha majeruhi na
vifo kadhaa.
Askari wamesema, basi hilo
limesababisha vifo vya watu 13 na majeruhi 80. Vyombo vingi vya habari
vimeripoti kuhusu tukio hilo.
Askari wamethibitisha kwamba,
hilo ni shambulio la Ugaidi.
Waziri mkuu wa Hispania,
Mariano Rajoy Brey akitumia mtandao wa ‘twitter’, amewapa pole majeruhi wote na
kuwataka askari wafanye kazi kwa weredi ili kuhakikisha wahalifu hao wanatiwa
nguvuni.
Wamiliki wa vyombo vya
usafiri wameomba kusitisha usafiri katika eneo lilipotokea shambulio na
wanawaomba watu wasikae mahali hapo.
Pia, askari wamewaomba watu
wote kutokutuma picha za shambulio hususani zile zinazowaonesha majeruhi.