Kiswahili pre NECTA 4
SEHEMU A (alama 10)
1. Soma kifungu cha habari ifuatayo kisha
jibu maswali kama ilivyoelekezwa.
Mako, mwosha magari maarufu mtaani Sakubimbi, alishughulika
kama kawaida yake. Leo alionekana kuchoka zaidi, pengine tenda ya kuosha Fuso,
ilimnyong’onyeza vilivyo. Mwanaume huyu alikuwa na mwili wa wastani tu,
kakamavu aliyezifikia kilo 61 kwenye uzani.
Wakati akiendelea kuosha Fuso ile, jua liliendelea kuipiga ngozi yake,
naye hakuisha kushika nywele, kipilipili kilichokoza, ngumu zimerundikana na
kutengeneza kitu kama mkutano wa nzi, labda hazikuliona chanuo kwa muda!
Fuso sasa ilitakata haswaa, Mako
akatembea mpaka alipo mwajiri wake, akachukua fedha na kuzielekeza kibindoni,
kabla hazijafika akastushwa na sauti yenye kitetemeshi cha kuigiza,
“Uko chini ya ulinzi, toa fedha
uishi…”
Mako akabinua bichwa ili apate kumtazama aliyetema maneno hayo, macho yake
yakagongana na sura ya mtoto mdogo, umri miaka saba, kavaa sare za shule na
begi dogo kalipachika mgongoni, kisha akambeba kindakindaki. Kwa ambae
angewaona hata kama angekuwa mgeni eneo hilo ni lazima angegundua kuwa viumbe
wale walikuwa ni mtu na mwanae. Nkenye alifanana mno na baba yake, hasa zile
nywele, kipilipili kilichokoza. Majirani walisema Nkenye alijaa urumbi wa
maneno kama babaye.
MASWALI
i.
Andika
kichwa cha habari hiyo kwa maneno yasiyopungua matano.
ii.
Ni
kazi gani alifanya Mako?
iii.
Nini
maana ya neno kibindoni?
iv.
Kwa
nini watu walisema kuwa Mako alifanana na mwanaye?
v.
Taja
mafunzo mawili yanayopatikana katika habari hiyo?
2. Andika ufupisho wa aya ya mwisho kwa
maneno yasiyozidi 30.
SEHEMU B (alama 25)
3. Katika kila moja ya sentensi zifuatazo,
onesha kosa moja la kisarufi kisha andika sentensi hiyo kwa usahihi.
a) Kinyonga kinakimbia. b) Arusi ya dada
yenu zitakuwa Disemba 2015.
c)
Mwaka
huu jua zinachoma sana. D) Tafadhali nikope shilingi mia nitakurudishia kesho kutwa.
e)
Kichumba
hiki kichafu sana.
4. Onesha dhima ya kiambishi “ni”
kilichopigiwa msitari katika sentensi zifuatazo.
a. alinisaidia b. wajumbe wapo mkutanoni
c.wakubalieni d. yeye ni mvivu e. nina kalamu
SEHEMU C (alama 10)
5. Eleza tofauti iliyopo kati ya hotuba na
risala. Andika hotuba kuhusu “Maji ni Uhai.”
SEHEMU D (alama 10)
6. Eleza jinsi shughuli za Waarabu
zilivyosaidia kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili nchini Tanzania kabla ya
uhuru.
SEHEMU E (alama 45)
7. “mwandishi wa fasihi ni mchunguzi wa
jamii ambaye huyaweka wazi maovu mbalimbali”. Jadili jinsi kazi za washairi
wawili kati ya hao walioorodheshwa zilivyosadifu kauli hii.
8. “Msanii ni mwalimu wa jamii”.
Thibitisha kauli hii kwa kutumia riwaya mbili ulizosoma.
9. Tunga utenzi wenye beti nne kuhusu
umuhimu wa maji.